Wageni
walipokuja pwani ya Afrika mashariki waliwakuta wenyeji tayari wana lugha yao
ya mawasiliano ambayo ni Kiswahili na pia lugha hiyo ilikuwa inatumika katika
shughuli za kibiashara miongoni mwao.
Kwahiyo wageni walipofika pwani ya Afrika
mashariki hawakuona sababu ya kutumia lugha nyingine zaidi ya Kiswahili katika
shughuli zao mbalimbali.
pia
wageni waliofika pwani ya Afrika mashariki, walifika kwa nyakati tofauti
tofauti na walifika wageni kama vile waarabu, wareno, wajerumani na waingereza
na wageni hawa kuna baadhi walikiendeleza Kiswahili na wengine walikidumaza
Kiswahili
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI ENZI
ZA WAARABU
Swali: Eleza mambo mbalimbali yaliyo changia ukuaji na ueneaji wa kiswahili nchini Tanzania wakati wa utawala wa waarabu.
Kuenea
kwa lugha ni kuongozeka kwa watumiaji. Wageni wa kwanza kuja pwani ya Afrika mashariki
ni waarabu na kutokana na kuingiliana na wabantu katika Nyanja mbalimbali
Kiswahili kilichukuliana maneno na kuathiriana na lugha ya kiarabu
Sababu zilizochangia kukua kwa
Kiswahili enzi za waarabu
·
Biashara
–
Waarabu walipowasili katika mwambao wa pwani ya Afrika mashariki walianza
kufanya biashara na wabantu. Kutokana na maingiliano hayo Kiswahili kilianza
kupanuka na kuongozeka misamiati kwa hiyo bila shaka Kiswahili kilikuwa
kutokana na maingiliano hayo. Mfano wa msamiati uliochukuliwa katoka kwa
waarabu ni kama vile jahazi, kodi, adesii n.k
· Utawala
–
waarabu pia walitumia Kiswahili katika shughuli mbalimbali za kiutawala.
Waarabu walitawala Zanzibar, sehemu za pwani ya bara na pemba kutokana na shughuli za kiutawala kuna maneno ya kiarabu ambayo yameingia kwenye Kiswahili. Mfano; mwinyi, sultani, mtukufu, enzi n.k
Waarabu walitawala Zanzibar, sehemu za pwani ya bara na pemba kutokana na shughuli za kiutawala kuna maneno ya kiarabu ambayo yameingia kwenye Kiswahili. Mfano; mwinyi, sultani, mtukufu, enzi n.k
·
Dini
– Hali kadhalika walipowasili walianzisha dini yao ya kiislamu kwenye upwa wa
Afrika kwa kutumia lugha ya Kiswahili. Waafrika walifundishwa kuandika na
kusoma kwa hati za kiarabu ili waweze kusoma na kuelewa kurani.
Hivyo wakajikuta wanaingiza baadhi ya maneno ya kiarabu kwenye lugha ya Kiswahili. Baadhi ya maneno ni kama vile elimu, alasiri, alfajiri n.k
Hivyo wakajikuta wanaingiza baadhi ya maneno ya kiarabu kwenye lugha ya Kiswahili. Baadhi ya maneno ni kama vile elimu, alasiri, alfajiri n.k
· Ndoa
– wageni hawa pia walipofika pwani ya Afrika mashariki waliishi kwa miaka mingi
na hivyo kuchangamana na wenyeji na baadae waarabu wakaoa wanawake wa kibantu
na hata vizazi vyao vilipozaliwa.
Walitumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano yao na pia hata utamaduni wao ulijiegemeza kwenye lugha ya Kiswahili. Hata jamii ya watu wa pwani waliwaita watoto wao waswahili badala ya maneno kama vile chotara, kwahiyo kutokana na hivyo basi ndoa kati ya waarabu na wabantu ulichangia kwa kiasi kikubwa kukua na kuenea kwa waswahili
Walitumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano yao na pia hata utamaduni wao ulijiegemeza kwenye lugha ya Kiswahili. Hata jamii ya watu wa pwani waliwaita watoto wao waswahili badala ya maneno kama vile chotara, kwahiyo kutokana na hivyo basi ndoa kati ya waarabu na wabantu ulichangia kwa kiasi kikubwa kukua na kuenea kwa waswahili
KUKUA NA KUENEA KWA KISWAHILI ENZI
ZA UTAWALA WA WAJERUMANI NCHINI TANZANIA
Swali: Eleza shughuli za wajerumani zilizo saidia kukua na kueneza kiswahili nchini Tanzania
Wajerumani
pia walitawala Tanganyika kwa muda wa miaka 30 na walipofika walikuta Kiswahili
kimekua sana katika nchi za Afrika mashariki kwahiyo walipofika Tanganyika
walitumia lugha ya Kiswahili kama chombo cha mawasiliano katika shughuli zao
mbalimbali za utawala na hata kwenye kutolea elimu kwa ajili ya manufaa yao.
Pia
mfanyakazi yeyote wa kiafrika ili kupata kazi ilimbidi ajue Kiswahili kwa
kuongea na kuandika ndipo apate kazi pia ripoti zote za utawala wa kijerumani
zilitakiwa kuandikwa kwa Kiswahili.
Vilevile
wanafunzi waliohitimu walisambazwa sehemu mbalimbali nchini na kwa njia hiyo
kiswahili kilikua na kuenea sana halikadhalika mashamba yaliyoanzishwa na
wajerumani yalikuwa na wafanyakazi mchanganyiko kutoka sehemu mbalimbali na
lugha ya mawasiliano miongoni mwao ilikuwa ni kiswahili kwa hiyo walichukua na
baadhi ya msamiati kutoka kwenye kabila zao na kuingiza kwenye Kiswahili na
hivyo kuchangia ukuaji wa Kiswahili
MBINU ZILIZOTUMIKA KUENEZA KWA
KISWAHILI NCHINI TANZANIA WAKATI WA UTAWALA WA WAJERUMANI
Mahakama
– utawala wa kijerumani ulitumia pia lugha ya Kiswahili katika shughuli zake
kwa hivyo kazi zote ziliendeshwa kwa lugha ya Kiswahili na pia wafanyakazi na
wazee na mahakani walihoji na kutoa hukumu kwa watuhumiwa kwa kutumia lugha ya
Kiswahili na hivyo kuchangia kukua na kuenea kwa lugha ya Kiswahili
Elimu –
mashuleni pia Kiswahili kilitumika kama lugha ya kufundishia na kijerumani
kilifundishwa kama somo la kawaida tu katika shule za msingi.
Wajerumani walijenga shule sehemu za tabora, ujiji, kilimatinda, mpwapwa, kasangu mwaka 1905, iringa, mwanza, bukoba, kilosa, tukuyu, na moshi pia vyuo vya kufundishia walimu vilianzishwa huko tabora na bukoba hivyo basi walimu na wanafunzi walijifunza na kukitumia Kiswahili katika shughuli zao za elimu na kusababisha kuenea na kukua kwa Kiswahili
Wajerumani walijenga shule sehemu za tabora, ujiji, kilimatinda, mpwapwa, kasangu mwaka 1905, iringa, mwanza, bukoba, kilosa, tukuyu, na moshi pia vyuo vya kufundishia walimu vilianzishwa huko tabora na bukoba hivyo basi walimu na wanafunzi walijifunza na kukitumia Kiswahili katika shughuli zao za elimu na kusababisha kuenea na kukua kwa Kiswahili
Utawala –
wajerumani walipofika nchini walikuta lugha ya Kiswahili imekua na kuenea sana
hivyo nao katika utawala na hivyo kuamua kujifunza Kiswahili kabla ya kuja
nchini na pia hapa nchini wajerumani walitoa mwongozo kwa viongozi wa nchini
kwa kutumia lugha ya Kiswahili na hivyo viongozi wote wa kiafrika mfano akida,
jumbe n.k walitakiwa kujifunza lugha ya Kiswahili kwasababu walikuwa wanatumwa
sehemu mbalimbali sio nchi walikozaliwa tu hivyo kuchangia kukua na kuenea kwa
haraka.
Shughuli za kilimo (mashamba)
– wajerumani pia walianzisha mashamba makubwa ya mazao ya biashara na
kuwalazimisha watu wafanye kazi kwenye mashamba hayo mfano, mashamba ya katani
Tanga, kahama, Kilimanjaro kwahiyo kwenye mashamba hayo kulikuwa na idadi kubwa
ya watu kutoka sehemu mbalimbali na lugha yao ilikuwa ni Kiswahili kwahiyo wale
waliobahatika kurejea majumbani mwao walisaidia kukieneza Kiswahili kwasababu
waliendelea kutumia lugha ya kiswahili.